Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Waqi'ah ( The Event ) | Swahili
About Script
Surah Al-Waqi'ah ( The Event )

Swahili

Surah Al-Waqi'ah ( The Event ) - Aya count 96

إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ ﴿١﴾

Litakapo tukia hilo Tukio

لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ ﴿٢﴾

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

خَافِضَةٌۭ رَّافِعَةٌ ﴿٣﴾

Literemshalo linyanyualo,

إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّۭا ﴿٤﴾

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّۭا ﴿٥﴾

Na milima itapo sagwasagwa,

فَكَانَتْ هَبَآءًۭ مُّنۢبَثًّۭا ﴿٦﴾

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًۭا ثَلَٰثَةًۭ ﴿٧﴾

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

فَأَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ ﴿٨﴾

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

وَأَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ ﴿٩﴾

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ ﴿١٠﴾

Na wa mbele watakuwa mbele.

أُوْلَٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ ﴿١١﴾

Hao ndio watakao karibishwa

فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ ﴿١٢﴾

Katika Bustani zenye neema.

ثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ ﴿١٣﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَقَلِيلٌۭ مِّنَ ٱلْءَاخِرِينَ ﴿١٤﴾

Na wachache katika wa mwisho.

عَلَىٰ سُرُرٍۢ مَّوْضُونَةٍۢ ﴿١٥﴾

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَٰبِلِينَ ﴿١٦﴾

Wakiviegemea wakielekeana.

يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌۭ مُّخَلَّدُونَ ﴿١٧﴾

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

بِأَكْوَابٍۢ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍۢ مِّن مَّعِينٍۢ ﴿١٨﴾

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ ﴿١٩﴾

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

وَفَٰكِهَةٍۢ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ ﴿٢٠﴾

Na matunda wayapendayo,

وَلَحْمِ طَيْرٍۢ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ﴿٢١﴾

Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

وَحُورٌ عِينٌۭ ﴿٢٢﴾

Na Mahurulaini,

كَأَمْثَٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ ﴿٢٣﴾

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

جَزَآءًۢ بِمَا كَانُواْ يَعْمَلُونَ ﴿٢٤﴾

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًۭا وَلَا تَأْثِيمًا ﴿٢٥﴾

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

إِلَّا قِيلًۭا سَلَٰمًۭا سَلَٰمًۭا ﴿٢٦﴾

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

وَأَصْحَٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلْيَمِينِ ﴿٢٧﴾

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

فِى سِدْرٍۢ مَّخْضُودٍۢ ﴿٢٨﴾

Katika mikunazi isiyo na miba,

وَطَلْحٍۢ مَّنضُودٍۢ ﴿٢٩﴾

Na migomba iliyo pangiliwa,

وَظِلٍّۢ مَّمْدُودٍۢ ﴿٣٠﴾

Na kivuli kilicho tanda,

وَمَآءٍۢ مَّسْكُوبٍۢ ﴿٣١﴾

Na maji yanayo miminika,

وَفَٰكِهَةٍۢ كَثِيرَةٍۢ ﴿٣٢﴾

Na matunda mengi,

لَّا مَقْطُوعَةٍۢ وَلَا مَمْنُوعَةٍۢ ﴿٣٣﴾

Hayatindikii wala hayakatazwi,

وَفُرُشٍۢ مَّرْفُوعَةٍ ﴿٣٤﴾

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

إِنَّآ أَنشَأْنَٰهُنَّ إِنشَآءًۭ ﴿٣٥﴾

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

فَجَعَلْنَٰهُنَّ أَبْكَارًا ﴿٣٦﴾

Na tutawafanya vijana,

عُرُبًا أَتْرَابًۭا ﴿٣٧﴾

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

لِّأَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ ﴿٣٨﴾

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

ثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ ﴿٣٩﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَثُلَّةٌۭ مِّنَ ٱلْءَاخِرِينَ ﴿٤٠﴾

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

وَأَصْحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَٰبُ ٱلشِّمَالِ ﴿٤١﴾

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

فِى سَمُومٍۢ وَحَمِيمٍۢ ﴿٤٢﴾

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

وَظِلٍّۢ مِّن يَحْمُومٍۢ ﴿٤٣﴾

Na kivuli cha moshi mweusi,

لَّا بَارِدٍۢ وَلَا كَرِيمٍ ﴿٤٤﴾

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

إِنَّهُمْ كَانُواْ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ ﴿٤٥﴾

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ ﴿٤٦﴾

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ﴿٤٧﴾

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ ﴿٤٨﴾

Au baba zetu wa zamani?

قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْءَاخِرِينَ ﴿٤٩﴾

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ ﴿٥٠﴾

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلْمُكَذِّبُونَ ﴿٥١﴾

Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

لَءَاكِلُونَ مِن شَجَرٍۢ مِّن زَقُّومٍۢ ﴿٥٢﴾

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ ﴿٥٣﴾

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

فَشَٰرِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ ٱلْحَمِيمِ ﴿٥٤﴾

Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

فَشَٰرِبُونَ شُرْبَ ٱلْهِيمِ ﴿٥٥﴾

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ ٱلدِّينِ ﴿٥٦﴾

Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

نَحْنُ خَلَقْنَٰكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ ﴿٥٧﴾

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

أَفَرَءَيْتُم مَّا تُمْنُونَ ﴿٥٨﴾

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

ءَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلْخَٰلِقُونَ ﴿٥٩﴾

Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ ٱلْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ ﴿٦٠﴾

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَٰلَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِى مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٦١﴾

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ ﴿٦٢﴾

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

أَفَرَءَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ ﴿٦٣﴾

Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

ءَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلزَّٰرِعُونَ ﴿٦٤﴾

Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

لَوْ نَشَآءُ لَجَعَلْنَٰهُ حُطَٰمًۭا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ ﴿٦٥﴾

Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

إِنَّا لَمُغْرَمُونَ ﴿٦٦﴾

Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ ﴿٦٧﴾

Bali sisi tumenyimwa.

أَفَرَءَيْتُمُ ٱلْمَآءَ ٱلَّذِى تَشْرَبُونَ ﴿٦٨﴾

Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

ءَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ ٱلْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنزِلُونَ ﴿٦٩﴾

Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

لَوْ نَشَآءُ جَعَلْنَٰهُ أُجَاجًۭا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ ﴿٧٠﴾

Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

أَفَرَءَيْتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِى تُورُونَ ﴿٧١﴾

Je! Mnauona moto mnao uwasha?

ءَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَآ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنشِـُٔونَ ﴿٧٢﴾

Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

نَحْنُ جَعَلْنَٰهَا تَذْكِرَةًۭ وَمَتَٰعًۭا لِّلْمُقْوِينَ ﴿٧٣﴾

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ ﴿٧٤﴾

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

۞ فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ ﴿٧٥﴾

Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٌۭ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ﴿٧٦﴾

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٌۭ كَرِيمٌۭ ﴿٧٧﴾

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

فِى كِتَٰبٍۢ مَّكْنُونٍۢ ﴿٧٨﴾

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلْمُطَهَّرُونَ ﴿٧٩﴾

Hapana akigusaye ila walio takaswa.

تَنزِيلٌۭ مِّن رَّبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ ﴿٨٠﴾

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَفَبِهَٰذَا ٱلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ﴿٨١﴾

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

فَلَوْلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلْحُلْقُومَ ﴿٨٣﴾

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

وَأَنتُمْ حِينَئِذٍۢ تَنظُرُونَ ﴿٨٤﴾

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ ﴿٨٥﴾

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

فَلَوْلَآ إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ ﴿٨٦﴾

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

تَرْجِعُونَهَآ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ ﴿٨٧﴾

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ ﴿٨٨﴾

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

فَرَوْحٌۭ وَرَيْحَانٌۭ وَجَنَّتُ نَعِيمٍۢ ﴿٨٩﴾

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنْ أَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ ﴿٩٠﴾

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

فَسَلَٰمٌۭ لَّكَ مِنْ أَصْحَٰبِ ٱلْيَمِينِ ﴿٩١﴾

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ ﴿٩٢﴾

Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

فَنُزُلٌۭ مِّنْ حَمِيمٍۢ ﴿٩٣﴾

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ ﴿٩٤﴾

Na kutiwa Motoni.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلْيَقِينِ ﴿٩٥﴾

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ ﴿٩٦﴾

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.

Quran For All V5