Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Qiyamah ( The Resurrection ) | Swahili
About Script
Surah Al-Qiyamah ( The Resurrection )

Swahili

Surah Al-Qiyamah ( The Resurrection ) - Aya count 40

لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ ﴿١﴾

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ ﴿٢﴾

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ ﴿٣﴾

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ ﴿٤﴾

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ ﴿٥﴾

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَٰمَةِ ﴿٦﴾

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ ﴿٧﴾

Basi jicho litapo dawaa,

وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ ﴿٨﴾

Na mwezi utapo patwa,

وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ ﴿٩﴾

Na likakusanywa jua na mwezi,

يَقُولُ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ ﴿١٠﴾

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

كَلَّا لَا وَزَرَ ﴿١١﴾

La! Hapana pa kukimbilia!

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ ﴿١٢﴾

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

يُنَبَّؤُاْ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ ﴿١٣﴾

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

بَلِ ٱلْإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌۭ ﴿١٤﴾

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ ﴿١٥﴾

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ ﴿١٦﴾

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ ﴿١٧﴾

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

فَإِذَا قَرَأْنَٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ ﴿١٨﴾

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ ﴿١٩﴾

Kisha ni juu yetu kuubainisha.

كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ ﴿٢٠﴾

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

وَتَذَرُونَ ٱلْءَاخِرَةَ ﴿٢١﴾

Na mnaacha maisha ya Akhera.

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاضِرَةٌ ﴿٢٢﴾

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌۭ ﴿٢٣﴾

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌۭ ﴿٢٤﴾

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌۭ ﴿٢٥﴾

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ ﴿٢٦﴾

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍۢ ﴿٢٧﴾

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ ﴿٢٨﴾

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ ﴿٢٩﴾

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ ﴿٣٠﴾

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ ﴿٣١﴾

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿٣٢﴾

Bali alikanusha, na akageuka.

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ ﴿٣٣﴾

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ ﴿٣٤﴾

Ole wako, ole wako!

ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ ﴿٣٥﴾

Kisha Ole wako, ole wako!

أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى ﴿٣٦﴾

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

أَلَمْ يَكُ نُطْفَةًۭ مِّن مَّنِىٍّۢ يُمْنَىٰ ﴿٣٧﴾

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةًۭ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٣٨﴾

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ ﴿٣٩﴾

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْۦِىَ ٱلْمَوْتَىٰ ﴿٤٠﴾

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?

Quran For All V5