Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) | Swahili
About Script
Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out )

Swahili

Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) - Aya count 46

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا ﴿١﴾

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,

وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا ﴿٢﴾

Na kwa wanao toa kwa upole,

وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا ﴿٣﴾

Na wanao ogelea,

فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا ﴿٤﴾

Wakishindana mbio,

فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا ﴿٥﴾

Wakidabiri mambo.

يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ ﴿٦﴾

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,

تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ ﴿٧﴾

Kifuate cha kufuatia.

قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ ﴿٨﴾

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,

أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ ﴿٩﴾

Macho yatainama chini.

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ ﴿١٠﴾

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ ﴿١١﴾

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

قَالُواْ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ ﴿١٢﴾

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ ﴿١٣﴾

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ ﴿١٤﴾

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ ﴿١٥﴾

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى ﴿١٦﴾

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ ﴿١٧﴾

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ ﴿١٩﴾

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ ﴿٢٠﴾

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ ﴿٢١﴾

Lakini aliikadhibisha na akaasi.

ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ ﴿٢٢﴾

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ ﴿٢٣﴾

Akakusanya watu akanadi.

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْءَاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ ﴿٢٥﴾

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةًۭ لِّمَن يَخْشَىٰٓ ﴿٢٦﴾

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا ﴿٢٧﴾

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا ﴿٢٨﴾

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا ﴿٢٩﴾

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ ﴿٣٠﴾

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا ﴿٣١﴾

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا ﴿٣٢﴾

Na milima akaisimamisha,

مَتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ ﴿٣٣﴾

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ ﴿٣٤﴾

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ ﴿٣٥﴾

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ ﴿٣٦﴾

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ ﴿٣٧﴾

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا ﴿٣٨﴾

Na akakhiari maisha ya dunia,

فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ ﴿٣٩﴾

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ ﴿٤٠﴾

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ ﴿٤١﴾

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا ﴿٤٢﴾

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ ﴿٤٣﴾

Una nini wewe hata uitaje?

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ ﴿٤٤﴾

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا ﴿٤٥﴾

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا ﴿٤٦﴾

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.

Quran For All V5