Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah At-Takwir ( The Overthrowing ) | Swahili
About Script
Surah At-Takwir ( The Overthrowing )

Swahili

Surah At-Takwir ( The Overthrowing ) - Aya count 29

إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ ﴿١﴾

Jua litakapo kunjwa,

وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ ﴿٢﴾

Na nyota zikazimwa,

وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ ﴿٣﴾

Na milima ikaondolewa,

وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ ﴿٤﴾

Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ ﴿٥﴾

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ ﴿٦﴾

Na bahari zikawaka moto,

وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ ﴿٧﴾

Na nafsi zikaunganishwa,

وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ ﴿٨﴾

Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ ﴿٩﴾

Kwa kosa gani aliuliwa?

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ ﴿١٠﴾

Na madaftari yatakapo enezwa,

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ ﴿١١﴾

Na mbingu itapo tanduliwa,

وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ ﴿١٢﴾

Na Jahannamu itapo chochewa,

وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ ﴿١٣﴾

Na Pepo ikasogezwa,

عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ ﴿١٤﴾

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ ﴿١٥﴾

Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ ﴿١٦﴾

Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ ﴿١٧﴾

Na kwa usiku unapo pungua,

وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ ﴿١٨﴾

Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ ﴿١٩﴾

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ ﴿٢٠﴾

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ ﴿٢١﴾

Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ ﴿٢٢﴾

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ ﴿٢٣﴾

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ ﴿٢٤﴾

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ ﴿٢٥﴾

Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ ﴿٢٦﴾

Basi mnakwenda wapi?

إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ ﴿٢٧﴾

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ ﴿٢٨﴾

Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ ﴿٢٩﴾

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Quran For All V5