Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Burooj ( The Big Stars ) | Swahili
About Script
Surah Al-Burooj ( The Big Stars )

Swahili

Surah Al-Burooj ( The Big Stars ) - Aya count 22

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ ﴿١﴾

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ ﴿٢﴾

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

وَشَاهِدٍۢ وَمَشْهُودٍۢ ﴿٣﴾

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

قُتِلَ أَصْحَٰبُ ٱلْأُخْدُودِ ﴿٤﴾

Wameangamizwa watu wa makhandaki

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ ﴿٥﴾

Yenye moto wenye kuni nyingi,

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌۭ ﴿٦﴾

Walipo kuwa wamekaa hapo,

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌۭ ﴿٧﴾

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

وَمَا نَقَمُواْ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ ﴿٨﴾

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍۢ شَهِيدٌ ﴿٩﴾

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُواْ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ ﴿١٠﴾

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ جَنَّٰتٌۭ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ ﴿١١﴾

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ ﴿١٢﴾

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ ﴿١٣﴾

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ ﴿١٤﴾

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ ﴿١٥﴾

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

فَعَّالٌۭ لِّمَا يُرِيدُ ﴿١٦﴾

Atendaye ayatakayo.

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ ﴿١٧﴾

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ ﴿١٨﴾

Ya Firauni na Thamudi?

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِى تَكْذِيبٍۢ ﴿١٩﴾

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ ﴿٢٠﴾

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

بَلْ هُوَ قُرْءَانٌۭ مَّجِيدٌۭ ﴿٢١﴾

Bali hii ni Qur'ani tukufu

فِى لَوْحٍۢ مَّحْفُوظٍۭ ﴿٢٢﴾

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

Quran For All V5