Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-A'la ( The Most High ) | Swahili
About Script
Surah Al-A'la ( The Most High )

Swahili

Surah Al-A'la ( The Most High ) - Aya count 19

سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى ﴿١﴾

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,

ٱلَّذِى خَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٢﴾

Aliye umba, na akaweka sawa,

وَٱلَّذِى قَدَّرَ فَهَدَىٰ ﴿٣﴾

Na ambaye amekadiria na akaongoa,

وَٱلَّذِىٓ أَخْرَجَ ٱلْمَرْعَىٰ ﴿٤﴾

Na aliye otesha malisho,

فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحْوَىٰ ﴿٥﴾

Kisha akayafanya makavu, meusi.

سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ ﴿٦﴾

Tutakusomesha wala hutasahau,

إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ ﴿٧﴾

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.

وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٨﴾

Na tutakusahilishia yawe mepesi.

فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكْرَىٰ ﴿٩﴾

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.

سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ ﴿١٠﴾

Atakumbuka mwenye kuogopa.

وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلْأَشْقَى ﴿١١﴾

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,

ٱلَّذِى يَصْلَى ٱلنَّارَ ٱلْكُبْرَىٰ ﴿١٢﴾

Ambaye atauingia Moto mkubwa.

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ ﴿١٣﴾

Tena humo hatakufa wala hawi hai.

قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ ﴿١٤﴾

Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.

وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ ﴿١٥﴾

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا ﴿١٦﴾

Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!

وَٱلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ وَأَبْقَىٰٓ ﴿١٧﴾

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

إِنَّ هَٰذَا لَفِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ ﴿١٨﴾

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,

صُحُفِ إِبْرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ ﴿١٩﴾

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.

Quran For All V5