Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) | Swahili
About Script
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming )

Swahili

Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ ﴿١﴾

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ ﴿٢﴾

Siku hiyo nyuso zitainama,

عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ ﴿٣﴾

Zikifanya kazi, nazo taabani.

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ ﴿٤﴾

Ziingie katika Moto unao waka -

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ ﴿٥﴾

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ ﴿٦﴾

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ ﴿٧﴾

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ ﴿٨﴾

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ ﴿٩﴾

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ ﴿١٠﴾

Katika Bustani ya juu.

لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ ﴿١١﴾

Hawatasikia humo upuuzi.

فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ ﴿١٢﴾

Humo imo chemchem inayo miminika.

فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ ﴿١٣﴾

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ ﴿١٤﴾

Na bilauri zilizo pangwa,

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ ﴿١٥﴾

Na matakia safu safu,

وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ ﴿١٦﴾

Na mazulia yaliyo tandikwa.

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ ﴿١٧﴾

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ ﴿١٨﴾

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ ﴿١٩﴾

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ ﴿٢٠﴾

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ ﴿٢١﴾

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ ﴿٢٢﴾

Wewe si mwenye kuwatawalia.

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ ﴿٢٣﴾

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ ﴿٢٤﴾

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ ﴿٢٥﴾

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم ﴿٢٦﴾

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Quran For All V5