Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Balad ( The City ) | Swahili
About Script
Surah Al-Balad ( The City )

Swahili

Surah Al-Balad ( The City ) - Aya count 20

لَآ أُقْسِمُ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ﴿١﴾

Naapa kwa Mji huu!

وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ﴿٢﴾

Nawe unaukaa Mji huu.

وَوَالِدٍۢ وَمَا وَلَدَ ﴿٣﴾

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِى كَبَدٍ ﴿٤﴾

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌۭ ﴿٥﴾

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًۭا لُّبَدًا ﴿٦﴾

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ ﴿٧﴾

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ ﴿٨﴾

Kwani hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانًۭا وَشَفَتَيْنِ ﴿٩﴾

Na ulimi, na midomo miwili?

وَهَدَيْنَٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ ﴿١٠﴾

Na tukambainishia zote njia mbili?

فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ ﴿١١﴾

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ ﴿١٢﴾

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

فَكُّ رَقَبَةٍ ﴿١٣﴾

Kumkomboa mtumwa;

أَوْ إِطْعَٰمٌۭ فِى يَوْمٍۢ ذِى مَسْغَبَةٍۢ ﴿١٤﴾

Au kumlisha siku ya njaa

يَتِيمًۭا ذَا مَقْرَبَةٍ ﴿١٥﴾

Yatima aliye jamaa,

أَوْ مِسْكِينًۭا ذَا مَتْرَبَةٍۢ ﴿١٦﴾

Au masikini aliye vumbini.

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوْاْ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْاْ بِٱلْمَرْحَمَةِ ﴿١٧﴾

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

أُوْلَٰٓئِكَ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ ﴿١٨﴾

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمْ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ ﴿١٩﴾

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

عَلَيْهِمْ نَارٌۭ مُّؤْصَدَةٌۢ ﴿٢٠﴾

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Quran For All V5