Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Ash-Shams ( The Sun ) | Swahili
About Script
Surah Ash-Shams ( The Sun )

Swahili

Surah Ash-Shams ( The Sun ) - Aya count 15

وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا ﴿١﴾

Naapa kwa jua na mwangaza wake!

وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا ﴿٢﴾

Na kwa mwezi unapo lifuatia!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا ﴿٣﴾

Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا ﴿٤﴾

Na kwa usiku unapo lifunika!

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا ﴿٥﴾

Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا ﴿٦﴾

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

وَنَفْسٍۢ وَمَا سَوَّىٰهَا ﴿٧﴾

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا ﴿٨﴾

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,

قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا ﴿٩﴾

Hakika amefanikiwa aliye itakasa,

وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا ﴿١٠﴾

Na hakika amekhasiri aliye iviza.

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ ﴿١١﴾

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا ﴿١٢﴾

Alipo simama mwovu wao mkubwa,

فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَٰهَا ﴿١٣﴾

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا ﴿١٤﴾

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

وَلَا يَخَافُ عُقْبَٰهَا ﴿١٥﴾

Wala Yeye haogopi matokeo yake.

Quran For All V5