Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-Layl ( The Night ) | Swahili
About Script
Surah Al-Layl ( The Night )

Swahili

Surah Al-Layl ( The Night ) - Aya count 21

وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ ﴿١﴾

Naapa kwa usiku unapo funika!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ ﴿٢﴾

Na mchana unapo dhihiri!

وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ ﴿٣﴾

Na kwa Aliye umba dume na jike!

إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ ﴿٤﴾

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ ﴿٥﴾

Ama mwenye kutoa na akamchamngu,

وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾

Na akaliwafiki lilio jema,

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

Tutamsahilishia yawe mepesi.

وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾

Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,

وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾

Na akakanusha lilio jema,

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾

Tutamsahilishia yawe mazito!

وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ ﴿١١﴾

Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?

إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ ﴿١٢﴾

Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

وَإِنَّ لَنَا لَلْءَاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ ﴿١٣﴾

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًۭا تَلَظَّىٰ ﴿١٤﴾

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!

لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى ﴿١٥﴾

Hatauingia ila mwovu kabisa!

ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١٦﴾

Anaye kadhibisha na kupa mgongo.

وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى ﴿١٧﴾

Na mchamngu ataepushwa nao,

ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍۢ تُجْزَىٰٓ ﴿١٩﴾

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.

إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

Naye atakuja ridhika!

Quran For All V5