Deprecated: Creation of dynamic property QuranForAll::$default_reader_aya is deprecated in /home4/quranfo1/public_html/includes/class.php on line 170
Surah Al-'alaq ( The Clot ) | Swahili
About Script
Surah Al-'alaq ( The Clot )

Swahili

Surah Al-'alaq ( The Clot ) - Aya count 19

ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ ﴿١﴾

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ ﴿٣﴾

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ ﴿٤﴾

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

عَلَّمَ ٱلْإِنسَٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥﴾

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَيَطْغَىٰٓ ﴿٦﴾

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ ﴿٧﴾

Akijiona katajirika.

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ ﴿٨﴾

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ ﴿٩﴾

Umemwona yule anaye mkataza

عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ ﴿١٠﴾

Mja anapo sali?

أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ ﴿١١﴾

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ ﴿١٢﴾

Au anaamrisha uchamngu?

أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ ﴿١٣﴾

Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ ﴿١٤﴾

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ ﴿١٥﴾

Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

نَاصِيَةٍۢ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍۢ ﴿١٦﴾

Shungi la uwongo, lenye makosa!

فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ ﴿١٧﴾

Basi na awaite wenzake!

سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ ﴿١٨﴾

Nasi tutawaita Mazabania!

كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩ ﴿١٩﴾

Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!

Quran For All V5